Header Ads Widget

Responsive Advertisement

AINA ZA MASHAIRI YA HIP-HOP KAMA FID Q AU NIKKI MBISHI 💯 works

 

KARIBU SANA KATIKA MUENDELEZO WA MAKALA YETU ILIYOPITA BOFYA HAPA KUSOMA KAMA BADO


Baada ya hapo twende sawa sasa.

 Uandishi Kama Wa FID Q au Nikki M ishi?


Ngoja Tuanze na hao Kwanza.


JINSI YA KUANDIKA KAMA FARID KUBANDA AU "FID Q" 





 "Nilipotoka mbali na ninaheshimu nilipo

sikuwa na umuhimu kihivyo stimu zikanipa elimu ya Biko

Kimaandiko kimistari.. hadi fans  wanascream nikirap..

sikuamini kama nina zali mpaka nilipoidream hiphop"


Hayo Ni mashairi Yanayopatikana katika wimbo wake wa MAFANIKIO

Aliofanya na Baraka D Prince 


  Hapo Fid ametumia DOUBLE RHYMES AU VINA DABO.


Maneno Kama 



ninaheshimu nilipo/elimu ya biko

wanascream nikirap/dream  hiphop



Nadhani hapo umepata PICHA ya ninachomaanisha.


Katika uandishi huu ambao pia wanatumia wasanii wakubwa Duniani Kama Marehemu Big L, Rapper Fat Joe Na Jadakiss huwa unatakiwa utafute Kwanza vina vya mwisho kuliko maneno ya mwanzo.


Chukulia mfano unataka kurap KUHUSU Ugumu wa maisha.


Tafuta maneno kama 


SHIDA /GIZA /MIDA/SHIBA/IBA 

NYINGI/PIMBI / WIZI/CHIZI/SIMBI


HALAFU ANDIKA MSTARI KWA MFANO INAWEZA KUWA 


"Mtaani hakuna kazi Ni SHIDA NYINGI..

Unaweza kuwa mwizi UKA-IBA SIMBI"


😁😁😁  Inasound POA?????


Hiyo Ni Mbinu ambayo ukiweza KUCHEZA nayo itakusaidia Sana katika uandishi wa Aina ya Fid Q.


Ushauri.


Sikiliza watu Kama P Mawenge,Nikki Mbishi, One,Srereo  n.k Kama unataka kujua uandishi huu.


SOMO LIJALO TUTAANGALIA JINSI YA KUANDIKA STORYTELLING RAP SONG


COMMENT HAPO CHINI ILI NIJUE KUWA TUPO PAMOJA


💪💪💪💪

Post a Comment

0 Comments